Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Mei 02, 2025 Local time: 19:21

Serikali ya Sudan yawakamata watu 41 kwa kumiliki vilipuzi


FILE - Jenerali Abdel Fattah al-Burhan
FILE - Jenerali Abdel Fattah al-Burhan

Mamlaka nchini Sudan inasema watu 41 wamekamatwa kwa kumiliki kiasi kikubwa cha vifaa vya milipuko.

Mwanasheria mkuu wa Sudan, Tagelsir al-Hebr, amewaambia waandishi wa Habari jana kuwa washukiwa walikuwa na vilipuzi vya kutosha kuuharibu mji mkuu, Khartoum.

Msemaji wa kikosi cha jeshi Rapid Support Forces, amesema uchunguzi wa Agosti juu ya harakati za makundi va kigaidi ulipelekea ukamataji huo.

Jamal Jumaa, amesema kuna wasi wasi baadhi ya raia wa Sudan, wataanza kulipua mabomu baada ya washukiwa kupatikana na shehena kubwa ya vilipuzi ambavyo vingeweza kusababisha uharibifu.

Wanalinganisha shehena za vilipuzi hivi sawa na mlipuko wa Lebanon uliotokea mwezi uliopita katika bandari ya Beirut, ambao uliua watu wasiopungua 190 na kuacha sehemu kubwa ya jiji ikiwa kifusi kutokana na mlipuko wa amonia nitrate.

XS
SM
MD
LG