Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 30, 2025 Local time: 05:37

Lebanon: Wakazi warejea maeneo ya mpakani, Israeli yaondoa baadhi ya wanajeshi


Wanajeshi wa Israeli wakitembea katika mpaka wa Israel na Lebanon Feb. 18, 2025.
Wanajeshi wa Israeli wakitembea katika mpaka wa Israel na Lebanon Feb. 18, 2025.

Wakazi wa Lebanon wamerudi katika makazi yao mpakani siku ya Jumatano, siku moja baada ya Israel kuondoa idadi kubwa ya wanajeshi wake kutoka sehemu hiyo.

Siku ya Jumanne, Februari 18 ndiyo ilikuwa siku ya mwisho kwa Israel kuondoa wanajeshi wake kutoka miji iliyo kusini mwa Lebanon, kulingana na makubaliano ya kusitisha vita yaliyosimamiwa na Marekani.

Makubaliano hayo yalimaliza mapigano kati ya Israel na wanamgambo wa Hezbollah, mwaka uliopita.

Israel imesema kwamba baadhi ya wanajeshi wake watasalia katika sehemu tano za mpaka huo, kwa maslahi ya usalama wa Israel.

Harakati za kikundi cha Kishia cha Hezbollah kimezuia barabara inayoelekea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beirut kupinga kuzuiwa kwa ndege mbili za Iran kutua hapo, huko Beirut Feb. 15, 2025.
Harakati za kikundi cha Kishia cha Hezbollah kimezuia barabara inayoelekea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beirut kupinga kuzuiwa kwa ndege mbili za Iran kutua hapo, huko Beirut Feb. 15, 2025.

Kundi la Hezbollah, ambalo lilipata pigo kubwa sana kwa kupoteza wapiganaji wake wakati wa vita, limesema Israel ilikuwa bado imekalia ardhi ya Lebanon na kwamba inaiwajibisha serikali ya Lebanon kuhakikisha wanajeshi wa Israel wanaondoka kabisa.

Forum

XS
SM
MD
LG